<abbr id="aakgw"><source id="aakgw"></source></abbr>
<dl id="aakgw"><tr id="aakgw"></tr></dl>
<li id="aakgw"></li>
  • <li id="aakgw"></li>
    <bdo id="aakgw"></bdo>
    <sup id="aakgw"><bdo id="aakgw"></bdo></sup><code id="aakgw"></code>

    Rais wa China atoa salamu za rambirambi kwa Rais wa Marekani kufuatia kufariki kwa Bw. Henry Kissinger

    (CRI Online) Desemba 01, 2023

    Rais wa China Xi Jinping siku ya Alhamisi ametoa salamu za rambirambi kwa Rais wa Marekani Joe Biden kufuatia kufariki kwa aliyekuwa waziri wa mambo ya nje wa Marekani Bw. Henry Kissinger.

    Katika salamu hizo, Rais Xi amesema China iko tayari kushirikiana na Marekani kuimarisha urafiki kati ya watu wa nchi hizo mbili, kuhimiza maendeleo mazuri ya uhusiano kati ya pande hizo mbili, ili kunufaisha wananchi wao, na kutoa mchango kadiri iwezavyo kwa amani na maendeleo ya dunia.

    (Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

    Picha