<abbr id="aakgw"><source id="aakgw"></source></abbr>
<dl id="aakgw"><tr id="aakgw"></tr></dl>
<li id="aakgw"></li>
  • <li id="aakgw"></li>
    <bdo id="aakgw"></bdo>
    <sup id="aakgw"><bdo id="aakgw"></bdo></sup><code id="aakgw"></code>

    Rais Xi na mkewe Peng Liyuan watoa salamu za Mwaka Mpya wa Jadi wa China kwa walimu, wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Lincoln ya Marekani

    (Tovuti ya Gazeti la Umma) Februari 14, 2024

    Beijing - Rais wa China Xi Jinping na mkewe, Peng Liyuan, wamejibu kadi ya salamu za Mwaka Mpya wa Jadi wa China siku ya Jumapili kutoka kwa walimu na wanafunzi wa Sekondari ya juu ya Lincoln ya Marekani, wakitoa salamu zao za heri za Mwaka wa Dragoni.

    Katika kadi ya salamu iliyotumwa kwa walimu na wanafunzi hao, Rais Xi na Peng wamewaalika kutembelea China mara nyingi zaidi, ikiwa ni pamoja na kushiriki katika programu zinazowaalika vijana 50,000 wa Marekani za mawasiliano na masomo nchini China, na kuchangia urafiki kati ya mataifa hayo mawili, hasa miongoni mwa vijana.

    Hapo kabla, walimu na wanafunzi wa shule katika Jimbo la Washington la Marekani walituma kadi ya salamu za Mwaka Mpya kwa Rais Xi, mkewe Peng na watu wa China, na kuwatakia heri na afya njema katika mwaka mpya wa jadi wa China. Walimu na wanafunzi zaidi ya 100 walitia saini kwenye kadi hiyo.

    (Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

    Picha