<abbr id="aakgw"><source id="aakgw"></source></abbr>
<dl id="aakgw"><tr id="aakgw"></tr></dl>
<li id="aakgw"></li>
  • <li id="aakgw"></li>
    <bdo id="aakgw"></bdo>
    <sup id="aakgw"><bdo id="aakgw"></bdo></sup><code id="aakgw"></code>

    Mwanariadha nyota wa Kenya Kipyegon katika matarajio ya kushinda medali za dhahabu

    (Tovuti ya Gazeti la Umma) Agosti 05, 2024

    Faith Kipyegon wa Kenya akishangilia baada ya kushinda katika fainali ya mbio za wanawake za mita 1500 wakati wa Michezo ya Olimpiki ya Tokyo 2020 kwenye Uwanja wa Olimpiki wa Tokyo Agosti 6, 2021. (Picha na Ben STANSALL/VCG)

    Faith Kipyegon wa Kenya akishangilia baada ya kushinda katika fainali ya mbio za wanawake za mita 1500 wakati wa Michezo ya Olimpiki ya Tokyo 2020 kwenye Uwanja wa Olimpiki wa Tokyo Agosti 6, 2021. (Picha na Ben STANSALL/VCG)

    Nairobi – Kenya inatarajia mavuno makubwa ya medali katika Michezo ya Olimpiki ya Paris kutoka timu yake mashuhuri ya wanariadha, lakini mwanariadha wake nyota Faith Chepngetich Kipyegon anaweza huhisi uzito zaidi juu ya mabega yake kuliko wengine, kwa kuwa anatarajiwa kushinda siyo medali moja bali mbili za dhahabu.

    Bingwa huyu mara mbili wa Michezo ya Olimpiki ya Rio de Janeiro 2016 na Tokyo 2020 kwa sasa ni nyota mkubwa zaidi wa timu ya Kenya wa mbio za kwenye njia za uwanjani, na anatarajiwa kuchukua medali nyingi zaidi huko Paris.

    Baada ya kuchelewesha kuanza kwa msimu huu kutokana jeraha la msuli wa paja, Kipyegon alithibitisha sifa yake ya kulinda ubingwa wa mbio za Olimpiki alipovunja rekodi yake mwenyewe ya mbio za mita 1500 kwa wanawake Julai 7.

    Shirikisho la Wanariadha Duniani Julai 27 liliidhinisha rekodi yake hiyo mpya, ambayo ni zawadi nzuri zaidi ya kumpeleka kwenye Olimpiki mama huyu mwenye fahari wa binti yake Aylin.

    Mkenya huyu atashindana katika mbio zote za mita 1,500 na za mita 5,000 katika michezo ya Olimpiki.

    Akizungumza na wanahabari wa China wiki mbili zilizopita, Kipyegon alisema hakuwa katika shinikizo kuelekea changamoto zake mbili hizo za Olimpiki, akisisitiza jambo pekee lililokuwa likimsumbua ni kudumisha utimamu wa afya kwa ajili ya mashindano.

    “Wakati ninapokuwa na afya nzuri ninajua jambo ninaloweza kufanya. Ninaweka mawazo yangu yote kuelekea kwenye michezo ya Olimpiki kwa sababu najua kutetea ubingwa si rahisi. Na ninatafuta kuwa kileleni kama bingwa mara tatu wa Olimpiki, ambayo siyo rahisi,” anasema.

    Safari yake ya kutoka mkimbiaji mwanafunzi katika mbio za kienyeji hadi kuwa nyota wa kimataifa kwa mara ya kwanza ilikuja kwenye uvutiaji wa ufuatiliaji duniani katika Mbio za Kuvuka Mashamba za Dunia 2010 zilizofanyika huko Bydgoszcz, Poland.

    Akiwa mkimbiaji wa bila kuvaa viatu, Kipyegon alinyakua medali ya dhahabu katika mbio za kilomita 6 kwa vijana wanawake, akianzisha kazi yake hiyo ya kitaaluma ambayo imemshuhudia akishinda medali 17 za dhahabu kwa Kenya ili kuwa mwanariadha wa kike mwenye mafanikio makubwa zaidi wa Kenya wa wakati wote.

    (Wahariri wa tovuti:Song Ge,Renato Lu)

    Picha